Huruma isiyo ya kawaida, Wema unaopita akili zetu, Rehema na Neema za ajabu, Vyote ni vya Mungu wetu!!

By  |  0 Comments

Jamani Mungu ana huruma, wema,neema,rehema,upendo sana,sana..rest assured, ukitafakari unaweza anza kulia tu hata kama ni mwanaume na haijalishi uwe ofisini,maombini, unaendesha gari,umelala,unatembea, unapika,unasoma, unalima huko village, uko bafuni unakoga, unaweza piga magoti huko huko hata haisumbui, maji ya mvua uyayokoga yanapoendelea kukumiminikia, unaweza anza kububujika na machozi ya furaha na kunena mara tu ukumbukapo wema na huruma za Mungu wetu , oooh! hata niandikapo sasa, nasikia mambo yanabadilika hapa, raha,furaha,uwepo na Roho Mt mwingi, nasikia vitu vinatekenya-tekenya kuleeee ndaniii… chumba cha ndani, allleluya… I love u so much Jesus my master, thank you so much God..my lovely dad jamani..love u dad and I worship u amen.

Maandiko:

Mwanzo. 19:12-25…..Malaika wa Bwana wanamsaidia hata kumshika mkono Lutu na wanae na mkewe ili kuwachangamsha watoroke haraka kabla ya moto kuangamiza,walimwambia afanye haraka haraka tena awatoe nje ya mji yeyote anayehusiana lakini ikawa kama anazubaaa ivi ikabidi malaika wawasaidie kufanya fasta kuchanja mbuga, jamani Mungu anahuruma..

Isaya 49:14-16…Mwanamke aliyezaa mwana inafahamika duniani kua ndiye mwenye huruma na upendo kuliko wote kwa mtoto hata inafahamika uchungu wa mwana aujua mzazi, mwanamke anaweza fanya lolote ili tu kumtetea mwana wa tumbo lake,atalala njaa,atauza vitumbua,matembele,atafukuzwa na mume, ataambiwa atoe mimba ili mapenzi yaendelee but yuko tayari kukosa yote kwa ajli ya mwanae,anaweza ingia ndani ya nyumba inawaka moto usio na ajizi kumuokoa mwanae kisha akatoka nae mtoto amemkumbatia akiwa mzima but yeye sura imeharibika beyond repair kwa kuunguzwa yet Mungu anasema kuna wakati mama huyo mzuri aweza kusahau huruma kwa mtoto wake mwenyewe na kutupilia mbali kule care yake kwa mwanae but si Mungu wetu…oooh my God, our God is indeed very unique jamani

Yona 4:1-11Mungu anahurumia mpaka ng’ombe,punda,pusi,farasi,kondoo,mbuzi, mbali na watu…jamani… can u imagine Mungu ana-care mpaka idadi kubwa ya mifugo na dog,kuku wakiwemo? angalia mstari wa 11.. Acheni Mungu aitwe Mungu

Yohana 13:1 na 15:13-14 Napenda tafsiri ya New King James ktk 13: 1 inasema ”He loved them to the end. wow!  yaani aliwapenda mpaka mwisho hahahaha alleluya..iyo tamu na ina nguvu sana na pia ktk 15:13….mtu anakupenda mpaka anayatoa maisha yake for u…sasa mtu akishakupenda mpaka mwisho na akakupenda mpaka kuhesabu uhai wake si kitu ili wewe na wewe tupone..jamani amebakiza nini sasa? nasikia machozi…anastahili mwokozi kupewa sifa na adhama na utukufu na hesima na kuabududiwa na shukurani...i love u so much Jesus

Mdo 9: 1-16 Mtu siku za nyuma kadhaa alikua anaua watu, sumbua kanisa,chinja wapendwa, vuruga-vuruga watu.kosesha raha wana wa Mungu eti ghafla mtu huyo huyo ambaye  ningekua mie ningeagiza malaika mmoja tu very junior kule juu aje kumchilia mbali kule msumbufu wa kanisa yule but ndio kwanza Yesu mzima zima anamtokea na kumpa  special task na title njema sana..tena anamu-address lovely positive..angalia mstari wa 15...da! Mungu huyu acheni tu…jamaa korofi ivyo na limetusumbua juzi tu Mdo 8:3 ndilo hilo  Mungu anali-pick na kulipa big huduma. yaani sina la kusema Mungu wetu bali uishi milele mfalme wetu mkuu.

Mdo 8:26-40 na 10: 1-48  Mungu mpaka ana-create plan ya kumuokoa/kumrehemu mtu, inabidi malaika atumwe kuongea na Philipo, then Roho Mt ana-direct step by step raketi..mdo. 8:29  then Philipo anakua nae  shap pia mstari wa 30-35, na pia Kornelio  akiwa hajaookoka but utoaji na maombi yake yalifanyika kumbukumbu mbinguniImagine Philipo baada ya mission kua accomplished akapata lift ya mbinguni mstari wa 39-40..imagine Kornelio is not saved but alikua mtoaji na muomba Mungu kila siku yaani raketi zote izi Mungu anaangaika ili awarehemu Kornelio na Mwafrika from Ethiopia

Wafilipi 2:5-11  Mtu yu namna ya Mungu,aliyekuwepo toka mwanzo, mwenye utukufu wa kutisha, mwenye mamlaka na enzi but yote hayo unayaweka kando kwanza then unakubali kuwa kama viumbe ulivyoviumba mwenyewe,kiushi nao miaka 30 ukiuza mpaka viti na meza za baba yako duniani, eti yote hayo ya kujishusha, kutojali spiritual personality yako unayafanya kwa ajli yetu tena tukiwa hatuna habari tunadunda tu na dhambi zetu huko mpaka baadae ndio tena Mungu akatuvuta tukaja kwako tukaokoka..taabu yote hiyo ya nini? kuacha enzi na mamlaka na kuja kudhalilishwa na viumbe hawa hawana adabu duniani!!!!!!!! jamani Yesu nakupenda sana,sana sijui nifanyeje mie ujue nakupenda mpenzi wa roho yangu?

Je unalo andiko/maandiko mengine ya kuonyesha huruma, rehema,neema,wema wa MUNGU, karibu utupie hapa,amen.

Amani ya Bwana Mungu iwe nanyi nyote amen.

Edwin Seleli

Share
Profile photo of Burundian Gospel

Share

You must be logged in to post a comment Login

Leave a Reply

error: Copyright reserved by The Shemeza Co. ©2017
Skip to toolbar